0
Maana ya Usimulizi
Ni dhana inayoelezea utoaji wa habari au hadithi kwa kutumia mdomo au maandishi.
Pia usimulizi huweza kuwa wa matukio mbalimbali kwa kuzingatia ufasaha wa Kiswahili yaani kiimbo, matamshi, sarufi na matumizi ya lugha
Aina za Usimulizi
(a).Usimulizi wa hadith
(b)Usimulizi wa habari
Usimulizi wa Hadithi
Ni masimulizi yenye lugha ya mjazo(nathari) na mtiririko wake huwa sahihi na rahisi, mara nyingi masimulizi huwa mafupi.
Kuna sifa zinatambulisha utambaji wa hadithi jukwaani, sifa hizo tunaposoma hatuwezi kupata kitabuni, sifa hizo ni Sauti ya utambaji ambayo husikika moja kwa moja na utambaji wa matukio kwenye jukwaa.
MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA HADITHI
Kujua muundo wa hadithi –Hadithi huwa ina sehemu tatu Mwanzo, Kati na Mwisho
Kwa mfano
Msimuliaji: Hadithi hadithi!
Wasikilizaji: Hadithi njoo uwongo njoo utamu kolea
Msimuliaji: Hapo zamani za kale
Wasikilizaji: Enheeeee(Wakiitikia)
Kwa mfano: Kuzaliwa….kukua…..kuoa.
Kisa kinachosimuliwa kinapaswa kuendana na maisha ya jamii husika
Kisa kinachosimuliwa kinapaswa kuendana na wakati.
Msimuliaji wa hadithi anapaswa kutumia lugha fasaha na matamshi sahihi ili wasikilizaji wapate kuelewa.
Mtumiaji atumie wahusika wanaoeleweka kwa wasikilizaji wake, Kwa mfano wahusika wanaweza kuwa wanyama kama vile sungura, fisi au twiga, Pia wanyama wanapaswa kupewa uhusika kulingana na matendo yao, kwa mfano sungura anawakilisha ujanja, simba anawakilisha ubabe na pundamilia anawakilisha uzuri
Msimuliaji anapaswa kutumia lugha ya picha ili aweze kuwavutia wasikilizaji wake, Kwa mfano; Simba alimtazama sungura kwa dharau…. Swala alikuwa anatembea kwa maringo…..simba aliponguruma ardhi yote ilitetemeka
Msimulizi pia anapaswa kutumia vitendo vya maigizo ili kuongeza uhai na msisimko katika hadithi inayosimuliwa, kwa mfano;sehemu ya hasira msimuliaji anapaswa kukunja sura ili kuonyesha hasira.
Msimuliaji pia anapaswa kupangilia matukio katika mtiririko unaofaa kuanzia mwanzo, kati na mwisho
SIFA ZA HADITHI SIMULIZI
DHIMA ZA HADITHI SIMULIZI
Huelimisha jamii, Husaidia jamii kuelewa mambo mbalimbali yaliyopo katika jamii yao
Kujenga jamii kwa kutoa maelezo m,balimbali kutoka kwenye hadithi
Hadithi husistiza ushirikiano katika jamii
Hadithi hurithisha busara toka kizazi kimoja kwenda kingine
Hadithi huburudisha jamii.
USIMULIZI WA HABARI
Ni maneno yanayotolewa na mtu au kundi la watu kuhusu jambo Fulani lililotokea au litakalotokea. Mara nyingi msimulizi wa habari huwa ni yule aliyeona tukio kwa mara ya kwanza au kusikia tukio likisimuliwa toka kwa mtu aliyeona kwa mara ya kwanza.
MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA USIMULIZI WA HABARI
Kutumia sauti inayosikika; sauti hutumiwa ili msikilizaji aweze kusikia na kuelewa vizuri kile kilichokusudiwa, Pia sauti huweka msistizo pale panapostahiki na kupambanua kauli.
Mpangilio mzuri wa mawazo; Huwezesha wasikilizaji kuelewa mtiririko wa habari au mawazo yanayotolewa
Kutumia lugha fasaha, msimuliaji anapaswa kumjua vizuri msikilizaji wake, wakati anaosimulia na mahali ili aweze kutumia maneno sahihi kulingana na wasikilizaji wake
Ni vizuri habari ikawa fupi ili isiwachoshe wasikilizaji.
Ni vizuri msimulizi kuwa na uhakika way ale anayoyasimulia, kwa kawaida kila habari huwa na ushahidi wa yale yanayosimuliwa.
Ni dhana inayoelezea utoaji wa habari au hadithi kwa kutumia mdomo au maandishi.
Pia usimulizi huweza kuwa wa matukio mbalimbali kwa kuzingatia ufasaha wa Kiswahili yaani kiimbo, matamshi, sarufi na matumizi ya lugha
Aina za Usimulizi
(a).Usimulizi wa hadith
(b)Usimulizi wa habari
Usimulizi wa Hadithi
Ni masimulizi yenye lugha ya mjazo(nathari) na mtiririko wake huwa sahihi na rahisi, mara nyingi masimulizi huwa mafupi.
Kuna sifa zinatambulisha utambaji wa hadithi jukwaani, sifa hizo tunaposoma hatuwezi kupata kitabuni, sifa hizo ni Sauti ya utambaji ambayo husikika moja kwa moja na utambaji wa matukio kwenye jukwaa.
MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA HADITHI
Kujua muundo wa hadithi –Hadithi huwa ina sehemu tatu Mwanzo, Kati na Mwisho
- Mwanzo
Kwa mfano
Msimuliaji: Hadithi hadithi!
Wasikilizaji: Hadithi njoo uwongo njoo utamu kolea
Msimuliaji: Hapo zamani za kale
Wasikilizaji: Enheeeee(Wakiitikia)
- Kati
Kwa mfano: Kuzaliwa….kukua…..kuoa.
- Mwisho
Kisa kinachosimuliwa kinapaswa kuendana na maisha ya jamii husika
Kisa kinachosimuliwa kinapaswa kuendana na wakati.
Msimuliaji wa hadithi anapaswa kutumia lugha fasaha na matamshi sahihi ili wasikilizaji wapate kuelewa.
Mtumiaji atumie wahusika wanaoeleweka kwa wasikilizaji wake, Kwa mfano wahusika wanaweza kuwa wanyama kama vile sungura, fisi au twiga, Pia wanyama wanapaswa kupewa uhusika kulingana na matendo yao, kwa mfano sungura anawakilisha ujanja, simba anawakilisha ubabe na pundamilia anawakilisha uzuri
Msimuliaji anapaswa kutumia lugha ya picha ili aweze kuwavutia wasikilizaji wake, Kwa mfano; Simba alimtazama sungura kwa dharau…. Swala alikuwa anatembea kwa maringo…..simba aliponguruma ardhi yote ilitetemeka
Msimulizi pia anapaswa kutumia vitendo vya maigizo ili kuongeza uhai na msisimko katika hadithi inayosimuliwa, kwa mfano;sehemu ya hasira msimuliaji anapaswa kukunja sura ili kuonyesha hasira.
Msimuliaji pia anapaswa kupangilia matukio katika mtiririko unaofaa kuanzia mwanzo, kati na mwisho
SIFA ZA HADITHI SIMULIZI
- Huhifadhiwa kwa kichwa na kutolewa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya masimulizi
- Hadithi simulizi mara nyingi hutumia wakati uliopita. Kwa mfano Hapo zamani za kale au zama zile za mabibi na mababu
- Hadithi simulizi huwa fupi na zenye kueleweka.
- Hadithi simulizi hutumia wahusika kama vile wanyama pia huweza kutumia wanadamu.
DHIMA ZA HADITHI SIMULIZI
Huelimisha jamii, Husaidia jamii kuelewa mambo mbalimbali yaliyopo katika jamii yao
Kujenga jamii kwa kutoa maelezo m,balimbali kutoka kwenye hadithi
Hadithi husistiza ushirikiano katika jamii
Hadithi hurithisha busara toka kizazi kimoja kwenda kingine
Hadithi huburudisha jamii.
USIMULIZI WA HABARI
Ni maneno yanayotolewa na mtu au kundi la watu kuhusu jambo Fulani lililotokea au litakalotokea. Mara nyingi msimulizi wa habari huwa ni yule aliyeona tukio kwa mara ya kwanza au kusikia tukio likisimuliwa toka kwa mtu aliyeona kwa mara ya kwanza.
MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA USIMULIZI WA HABARI
Kutumia sauti inayosikika; sauti hutumiwa ili msikilizaji aweze kusikia na kuelewa vizuri kile kilichokusudiwa, Pia sauti huweka msistizo pale panapostahiki na kupambanua kauli.
Mpangilio mzuri wa mawazo; Huwezesha wasikilizaji kuelewa mtiririko wa habari au mawazo yanayotolewa
Kutumia lugha fasaha, msimuliaji anapaswa kumjua vizuri msikilizaji wake, wakati anaosimulia na mahali ili aweze kutumia maneno sahihi kulingana na wasikilizaji wake
Ni vizuri habari ikawa fupi ili isiwachoshe wasikilizaji.
Ni vizuri msimulizi kuwa na uhakika way ale anayoyasimulia, kwa kawaida kila habari huwa na ushahidi wa yale yanayosimuliwa.